Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mtoto mkimbizi wa Syria huko Lebanon kupata cheti cha kuzaliwa kwa urahisi

Watoto wa shule katika shule moja kusini mwa Lebanon wakiwa darasani .Wengi wao ni ni atotowa wakimbizi kutoka Syria.Masharti ya kupata vyeti vya kuzaliwa yamelegezwa.
UNIFIL/Pasqual Gorriz
Watoto wa shule katika shule moja kusini mwa Lebanon wakiwa darasani .Wengi wao ni ni atotowa wakimbizi kutoka Syria.Masharti ya kupata vyeti vya kuzaliwa yamelegezwa.

Mtoto mkimbizi wa Syria huko Lebanon kupata cheti cha kuzaliwa kwa urahisi

Wahamiaji na Wakimbizi

Mabadiliko muhimu yaliyofanyika katika utaratibu wa  sheria za Lebanon kuhusu usajili wa watoto umewezesha  zaidi ya watoto  50,000 wakimbizi kutoka  Syria waliozaliwa Lebanon tangu mgogoro uanze  nchini mwao kuweza kusajiliwa. 

Kusini mwa Lebanon katika moja ya kambi za wakimbizi wa Syria.

Awali watoto wa wakimbizi wa Syria waliozaliwa hapa Lebanon na kukosa kusajiliwa ndani ya mwaka mmoja baada ya kuzaliwa, walipata taabu kupata cheti cha kuzaliwa.

Wazazi walipaswa kulipa hadi dola 1,500 ili kupata cheti, gharama ambayo ni ya juu na hawakuipatia umuhimu kutokana na mahitaji mengine ya lazima.

Watoto walikosa huduma muhimu kama afya na elimu.

 

Kundi la wakimbizi wa Syria wakiwa  mstarini tayari kuingia darasani huko Bar Elias nchini Lebanon
UNifeed Video
Kundi la wakimbizi wa Syria wakiwa mstarini tayari kuingia darasani huko Bar Elias nchini Lebanon

 

Mohammad al-Masry ni mkimbizi kutoka Syria.

“Siwezi kufanya lolote   kwa ajili ya mwanangu kisheria  bila ya kitabu cha familia. Inanilazimu kufanya hivyo nchini Syria , lakini ni vigumu kwenda huko hivi sasa.”

Hata hivyo hivi karibuni serikali ya Lebanon ilipitisha uamuzi ya kwamba watoto wote wa Syria waliozaliwa kati ya Januari Mosi 2011 na mwezi Machi 2018 wasajiliwe bila gharama yoyote.

Mohammad Jarjowi, ni afisa wa sheria wa kamati ya kimataifa ya uokozi IRC. 

“Sasa tunaweza kutayarisha vyeti vya kuzaliwa na kuvisajili katika masjala ya kigeni hata pale ambapo mtoto alikuwa  amepitisha ukomo wa usajili wa ndani ya mwaka mmoja tangu azaliwe.” 

 

Watoto wakimbizi kutoka Mali waliozaliwa kambi ya Mbera nchini Mauritania wakipatiwa hati ya cheti cha kuzaliwa.
UNHCR
Watoto wakimbizi kutoka Mali waliozaliwa kambi ya Mbera nchini Mauritania wakipatiwa hati ya cheti cha kuzaliwa.

 

Hatua hii imeokoa wakimbizi wengi kutoka Syria ambao watoto wao wamezaliwa ukimbizini Lebanon baada ya vita kuanza nchini mwao 2011.

Firaz ni mmoja wao na binti yake Yara Mimas ana umri wa miaka minne, kwake yeye shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limemletea nuru.

“UNHCR ilinisaidia kumsajili binti yangu binti yangu Yara. Usajili wake ulishakuwa umepitiliza kwa miaka mitatu.