Kutana na mkimbizi Fatima, raia wa Syria, na mumewe Abdel Kahar pamoja na watoto wao wadogo wanne ambao wanaishi katika shamba huko Sabha, Mafraq, kaskazini mwa Jordan. Wakati wa ufungaji mipaka kwa sababu ya COVID-19, Fatima hakuweza kufanya kazi shambani hali ambayo ilisababisha kupungua kwa kipato chake cha kawaida.