Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uhakika wa chakula ni mtihani mkubwa kwa watu wa jamii za asili: FAO

Watu wa jamii ya asili wanataka ardhi yao kwani ni zaidi ya kile ambacho watu wanafikiria
IIED- GEF Small Grants Programme, UNDP
Watu wa jamii ya asili wanataka ardhi yao kwani ni zaidi ya kile ambacho watu wanafikiria

Uhakika wa chakula ni mtihani mkubwa kwa watu wa jamii za asili: FAO

Wanawake

Uhakika wa chakula umeelezwa kuwa ni changamoto kubwa kwa watu wa jamii za asili hususan wanawake ambao ndio walezi wa familia na jamii.  

 Hayo ni kwa mujibu wa Yon Fernandez de Larrinoa ambaye ni kiongozi wa timu ya watu wa jamii za asili katika shirika la chakula na kilimo FAO.

Ameongeza kuwa  kuna jumla ya wanawake wa jamii za asili milioni 185 kote duniani ambao ni wavuvi, wawindaji, waokota matunda  na watetezi wa ardhi na rasilimali zao, lakini licha ya mchango wao mkubwa wa kiuchumi na kijamii mara nyingi wanatengwa na kutohusishwa katika mchakato wa kufanya maamuzi yanayowahusu.

Pia amesisitiza kuwa kuheshimu hali, na mchango wa watu wa jamii za asili ni muhimu kwani imekuwa kawaida kwa kazi zao kutothaminiwa, hawalipwi ujira unaostahili na wanadharauriwa kila wakati.