Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

watu wa asili

UNFPA Brazil/Isabela Martel

UN wawapongeza vijana wa jamii ya asili kwa kutokubali ukandamizaji wa jamii zao

Hii leo ni siku ya jamii ya watu wa asili duniani ambapo maudhui ni vijana, ikisherehekea vijana wa jamii ya asili na dhima yao katika kuleta mabadiliko na kuumba mustakabali wa dunia. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa ujumbe wake. 

Katika ujumbe wake wa siku hii iadhimishwayo tarehe 9 mwezi Agosti ya kila mwaka, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres anasema duniani kote watu wa jamii ya asili wanakabiliwa na changamoto, ardhi na rasilimali zao zikitishiwa haki zao zikikandamizwa na changamoto yao ya kila uchao ya kuenguliwa na kutengwa. 

Sauti
1'59"
UN Brazil

Amina J. Mohammed ziarani Amazon: Nimesikia maombi yenu na tutapaza sauti

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed anaendele ana ziara yake ya siku tano nchini Brazil ambapo siku ya Alhamisi Agosti 3, 2023 alizuru jamii ya watu wa asili ya Mapuera kwenye ukanda wa Amazon jimboni Para ambako huko alipata fursa ya kuzungumza na wanajamii hao na kusikia maombi yao, ziara ambayo anafanya kufuatilia utekelezaji wa malengo ya maendeleo endelevu, SDGs kuelekea mkutano wa viongozi kuhusu SDGs mwezi Septemba mwaka huu. Thelma Mwadzaya anatusimulia kilichojiri. 

Sauti
3'46"

04 AGOSTI 2023

Hii leo jaridani tunaangazia haki za binadamu na Akili Mnemba au ‘Artificial Intelligence’.  Makala tunakupeleka nchini Brazil na mashinani tutasikia ujumbe wa kijana kutoka Tanzania, salía papo hapo!  

Sauti
11'25"

26 APRILI 2023

Jaridani leo ripoti ya utalii wa milima na jamii ya watu wa asili wa Inuit.  Makala tunakuletea tunasalia hapa Makao Makuu na mashinani tunakupeleka Kisiwa cha Jamhuri ya Kiribati, kulikoni?

Sauti
10'57"
Herbert Angiki Nakimayak,Makamu wa rais wa baraza la jamii ya Inuit nchini humo anayehudhuria jukwaa la 22 la watu wa asili la Umoja wa Mataifa hapa Marekani alipozungumza na Idhaa hii ya Kiswahili.
UN News

Makazi ni moja ya changamoto kubwa kwa jamii ya watu wa asili wa Inuit wa Eskimo: Nakimayak

Jamii ya Inuit ya watu wa asili wa Eskimo ni miongoni mwa jamii za walio wachache sana kutoka jimbo la Inuvik nchini Canada. Jamii hiyo ambayo ina jumla ya watu 180,000 kwa asili ni ya wawindaji, wavuvi na wafugaji wa kuhamahama, lakini sasa kutokana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi wamelazimika kubadili mfumo wa maisha na kuishi mahali pamoja katika vijiji.

Sauti
2'33"

06 APRILI 2023

Hii leo jaridani tunakuletea mada kwa kina ambapo tunaangazia afya ya uzazi na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya afya ya uzazi salama kwa wanawake kutoka hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando Dk. Elieza Chibwe akizungumzia juu ya kukoma kwa hedhi kwa wanawake anasema “Ukihisi dalili za menopause mapema nenda hospitali.” Pia tunakuletea habari kwa ufupi zikiwemo salamu za sikukuu za Pasaka na Eid El Fitr kutoka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ombi la UNICEF la msaada kwa watoto waathirika wa matetemeko ya ardhi huko mashariki ya kati, na haki za watu wa jamii asili.

Sauti
13'2"
Elimu kwa lugha mama huwezesha wanafunzi kuziba pengo ya maisha kati ya nyumbani na shuleni.
UNISFA

Asilimia 40 ya wanafunzi duniani kote hawana fursa ya kusoma kwa lugha mama: UNESCO

Elimu itolewayo kwa wanafunzi kupitia lugha mama ikielezwa kuwa ni muhimu sio tu katika kuwezesha mtu kustawi na kuendelea bali pia kuhamisha urithi wa lugha, asilimia 40 ya wanafunzi duniani kote bado hawana fursa ya kufundishwa darasani kwa lugha yao wanaozungumza au wanaoelewa zaidi, amesema Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la elimu, sayansi na utamaduni, UNESCO, Audrey Azoulay katika ujumbe wake wa siku ya lugha mama duniani hii leo.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres (katikati) akutana na wanachama wa vyama vya ushirika vya kilimo vinavyoongozwa na wanawake na wanaume wazawa katika Kijiji cha Pierre Kondre-Redi Doti, katika ukanda wa msitu wa kitropiki wa Suriname.
UN Photo/Evan Schneider

Suriname inatoa “tumaini na msukumo kwa ulimwengu kuokoa misitu yetu ya mvua”: Mkuu wa UN

Suriname inaweza kuwa nchi ndogo na isiyo na watu wengi zaidi katika ukanda wa  Amerika ya Kusini, lakini ni moja ya nchi za kijani kibichi. Inachukuliwa kuwa kinara wa kimataifa katika uhifadhi wa bioanuwai, huku zaidi ya asilimia 90 ya ardhi yake ikifunikwa na misitu ya asili, rasilimali asilia isiyo na kifani ya taifa zaidi ya kufidia saizi yake.