Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake kwa njia ya video kuhusu siku ya leo ya watu wa asili ambayo huadhimishwa Agosti 9 ya kila mwaka, amesema ni muhimu kwa nchi kuandaa rasilimali ili kushughulikia mahitaji ya watu wa asili, kuheshimu michango yao na kuheshimu haki zao kujibu mahitaji yao, kuheshimu michango yao na kuheshimu haki zao zisizopingika.