Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ajira milioni 24 kubuniwa duniani ifikapo 2030-ILO.

'Bodaboda' za magurudumu matatu mjini Delhi India.Ripoti mpya ya ILO yasema  ajira milioni 24 kubuniwa ifikapo 2030
ILO/Vijay Kutty
'Bodaboda' za magurudumu matatu mjini Delhi India.Ripoti mpya ya ILO yasema ajira milioni 24 kubuniwa ifikapo 2030

Ajira milioni 24 kubuniwa duniani ifikapo 2030-ILO.

Ukuaji wa Kiuchumi

Ikiwa sera sawa za kukuza uchumi unaojali mazingira zitazingatiwa  ifikapo mwaka wa 2030, ajira takriban milioni 24 zitabuniwa.

Kulingana na ripoti ya shirika la kazi duniani ILOAjira duniani pamoja na mwelekeo wa kijamii 2018, kujali mazingira na kazi   iliyozinduliwa leo mjini Geneva, Uswisi ,hatua za kupunguza kiwango cha joto hadi nyuzi joto 2 katika kipimo cha selsiyasi, zitasababisha mazingira sawa ya kuunda ajira za kutosha ili kutoa pengo la ajira milioni 6 kwingineko.

Akizungumza wakati wa uzinduzi wa ripoti hiyo, Naibu Mkurugenzi Mkuu wa ILO, Deborah Greenfield, amesema kuwa matokeo ya ripoti yao yanatilia mkazo  kuwa ajira hutegemea  mazingira mazuri ya kiafya na huduma zinazotolewa.

Ameongeza kuwa uchumi unaojali mazingira unawezesha watu mamilioni zaidi kuondokana na umaskini, na kuwa na maisha bora kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Ripoti hiyo  inasema kuwa ajira mpya zitabuniwa  kwa kufuata mbinu endelevu katika sekta ya nishati ikiwemo mabadiliko kama vile kukuza matumizi ya magari yanayotumia umeme.

Bila kusahau mifumo ya huduma za ekolojia ikiwemo kusafisha hewa pamoja na maji, pembejeo, udhibiti wa wadudu waharibifu, kinga dhidi ya hali mbaya ya hali ya hewa pamoja na mengine mengi.

Pia uboreshaji wa sekta zingine kama uvuvi, kilimo, misitu na utalii ambavyo huajiri wafanyakazi bilioni 1.2, ikiwa utazingatiwa.

Hata hivyo ripoti hiyo kwa upande mwingine  inapiga mahesabu kuwa msongo kutokana na joto, utasababisha hasara ya asilimia 2 katika saa za  kazi ifikapo mwaka wa 2013 kutokana na watu kuugua.

Katika viwango vya kikanda bara la Asia litabuni ajira nyingi zaidi kuliko maeneo  mengine kwani zitakuwa milioni 14, na kufuatiwa na eneo la Amerika litakalobuni ajira milioni 3 na lile la pasifiki na Ulaya kuchukua nafasi ya tatu kwa  kiwango cha asilimia mbili.

Ripoti inaomba mataifa mengine yachukue hatua za kuwafundisha wafanyakazi  mbinu mbadala zinazohitajika kuelekea  uchumi usioharibu mazingira.