Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uamuzi wa mahakama Tanzania ni ushindi kwa umma- Balile

Picha: UNESCO
Uhuru wa kutumia mitandao.

Uamuzi wa mahakama Tanzania ni ushindi kwa umma- Balile

Haki za binadamu

Nchini Tanzania hii leo Mahakama Kuu kanda ya Mtwara imezuia kwa muda kuanza kwa matumizi ya kanuni mpya za maudhui ya mtandao nchini humo.

Kanuni hizo ambazo zilitakiwa kuanza kutumika rasmi tarehe 5 mwezi huu, zinataka pamoja na mambo mengine wamiliki wa blogu au watu wanaochapisha habari mtandaoni wawe wamesajiliwa, usajili ambao unafanyika kwa gharama.

Nimezungumza na Deodatus Balile, Kaimu Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri nchini Tanzania, TEF, ambao ni mmoja wa wadau sita waliowasilisha ombi la sitisho hilo mahakamani ambapo nimeanza kwa kumuuliza jinsi walivyopokea uamuzi huo.

(Mahojiano na Deodatus Balile)

Taasisi nyingine zilizowasilisha ombi hilo ni Legal and Human Rights Center (LHRC), Tanzania Human Rights Defenders (THRD), Media Council of Tanzania (MCT), Jamii Media, na Tanzania Media Women Association (TAMWA).

Katika kesi yao ya msingi ya mapitio ya kanuni hizo itakayoanza kusikilizwa tarehe 10 mwezi huu, taasisi hizo zimewashtaki Waziri wa Habari, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania na Mwanasheria Mkuu wa Serikali.

Wadau hao pamoja na mambo mengine wamesema kanuni zinakiuka kanuni za usawa, na zinapingana na haki ya kujieleza na haki ya usiri.