Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Umoja wa Mataifa wazindua mikakati ya kuzuia unyanyasaji  kingono na kuuzwa watoto

Wanafunzi nchini Sudan Kusini wakigiza suala la ukatili wa kingono katika maeneo yenye mizozo.
UNMISS/Isaac Billy
Wanafunzi nchini Sudan Kusini wakigiza suala la ukatili wa kingono katika maeneo yenye mizozo.

Umoja wa Mataifa wazindua mikakati ya kuzuia unyanyasaji  kingono na kuuzwa watoto

Haki za binadamu

Kamati ya Umoja wa Mataifa ambayo inafutilia haki za watoto inazinduliwa rasmi leo Alhamisi ikiwa na malengo  ya kusaidia nchi kutekekeza makubaliano  yanayohusu kuuzwa kwa watoto, watoto kutumiwa katika umalaya na biashara ya picha za uchi za watoto.

Maelekezo hayo yaliandikwa na  Kamati ya Umoja wa Mataifa inayohusika na haki za mtoto inaangazia sana vitisho vipya vinavyowalenga watoto kote duniani  kutonana na teknolojia ya kidijitali kama intaneti  na mitandao ya kijamii.

Kuboreka kwa teknolojia ya mawasiliano imewapa fursa mpya wanyanyasaji wa kimapenzi na njia za kuwadhulumu watoto. Zinatumiwa kuwavutia watoto kujiunga katika masuala ya ngono kwa njia ya video zinazotangazwa moja kwa moja mitandaoni.

Waendesha uovu huo huwasiliana na kubadilishana habari huku wakitumia mitandao ya siri kutekeleza vitendo hivyo.

Hii imekuwa changamoto mpya na ngumu kwa idara za sheria. Katika ulimwengu ambao matumizi ya mitandao ni kitu kinazidi kukua kwa kasi, tisho la watoto kunyanyaswa kingono au kununuliwa na kuuuzwa kama bidhaa ndani ya nchi ni nje imekuwa ikiongezeka kwa kasi sana. 

Miongozo hiyo ina lengo la kuleta uelewa zaidi wa mpango huo wa Umoja wa Mataifa na kutoa suluhu mwafaka kuambatana na changamoto ambazo nchi zimekabiliana nazo katika utekelezwaji wake.

Inalenga kusaidia  nchi 176 ambazo zimetia sahihi mpangilio huo na pia zile zitakazojiunga nao baadaye.