Tutawekeza kwa wasichana ili kujenga taifa thabiti: Tanzania
Siku ya kiamataifa ya idadi ya watu imeadhimishwa nchini Tanzania jijini Dar es salaam kwa tukio maalum hii leo, ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu nchini humo UNFPA limesisitiza umuhimu wa taifa hilo kuwekeza kwa wasichana vigori kwa maendeleo ya taifa.
Kwa upande wake mwakilishi wa serikali waziri wa afya, maendeleo ya jamii, wazee na watoto wa Tanzania Ummy Mwalimu amesema ili kujenga mustakabali wa nchi, uwekezaji kwa wasichana ni nyenzo isiyokwepeka kwani.
(SAUTI UMMY)
Kwa upande wao wadau wa masuala ya kijamii hususani asasi za kutetea wasichana na wanawake zimesisitiza elimu kwa jamii kuhusu kuwajali na kuwatahamini wasichana.