Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Maisha ya upweke kwa wakimbizi wa Syria nchini Lebanon

Maisha ya upweke kwa wakimbizi wa Syria nchini Lebanon

Mwaka wa sita sasa mzozo wa Syria unaendelea bila ya nuru ya kupata suluhu la kisiasa. Raia wa Syria wamekimbia makazi yao na wamesalia wakimbizi wa ndani na wengi wao wamesaka hifadhi nchi jirani na wengine kuvuka bahari na majangwa  hadi Ulaya. Miongoni mwao ni Jawaher ambaye sasa anaishi Lebanon. Raha ya maisha aliyozoea nchini mwake Syria imegeuka shubiri ambayo hata hana uhakika lini tena itakuwa tamu. Je kulikoni? Assumpta Massoi anafafanua kwenye makala hii.