MONUSCO yasihi vikundi vyenye silaha kuzisalimisha
Ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo MONUSCO umerejelea wito wa kuvitaka vikundi vyenye silaha nchini humo kusalimisha silaha hizo kwa ujumbe huo.
Akizumgumza katika mkutano wa waandishi wa habari na kunukuliwa radio washirika Okapi mkuu wa MONUSCO wilayani Ituri, M’hand Ladjouzi amesema ofisi hiyo kwa kushirikiana na serikali ya DRC iko mbioni kuanzisha tena mpango wa kuwapokea wenye silaha na kuonya kuwa kama vikundi hivyo havitaikitikia wito huo vitapokonywa silaha.
(Sauti Ladjzouzi)