IOM yapeleka msaada wa chakula visiwa vya Marshall
Visiwa vya Marshall vimekumbwa na ukame mkali kwa muda mrefu, hata hivyo japo hivi sasa mvua zinanyesha lakini chakula bado ni haba katika maeneo yaliyoathirika sana hususan yale ya kandokando na visiwa hivyo.
Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM limeanza kupeleka msaada wa chakula wa tani 45 kwa kaya 677 visiwani humo kwa njia ya anga na bahari. Jumbe Omari Jumbe ni msemaji wa IOM
(SAUTI YA JUMBE OMARI JUMBE)