Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Bunge la Urusi litupilie mbali muswada wa propaganda za ushoga.

Bunge la Urusi litupilie mbali muswada wa propaganda za ushoga.

Kundi la wataalamu huru wa masuala ya haki za kibinadamu la Umoja wa Mataifa limetoa wito kwa bunge la Urusi kutupilia mswada  ambao utaidhinisha kutolewa kwa adabu kwa propaganda zozote zinazohusu ushoga kwa watoto.

Wataalamu hao wanaonya kuwa mswada huo utakandamiza haki za binadamu nchini Urusi na kuwalenga zaidi walio mashoga , wasagaji na wale wanaobadili jinsia zao ambao tayari wamelegwa pakubwa nchini humo.

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya watetesi wa haki za binadamu Margaret Sakaggya ameonya kuwa sheria hiyo itatumika kukandamiza shughuli za wale wanaotetea haki za mashoga , wasagaji na wale wanaobadili jinsia zao. Wataalamu hao wanasema kuwa bado kuna fursa ya  kubadilisha mswada huo wakati itakaposomwa bungeni akiwataka wabunge kuutupilia mbali mswada huo ili kuhakikisha kuwepo kwa haki za binadamu nchini Urusi.