Kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya utoaji Huduma za Kibinadamu
Huku siku ya kimataifa ya utoaji wa huduma za kibinadamu ikisherehekewa tarehe 19 mwezi huu Umoja wa Mataifa umechukua hatua ya kutaka kufahamu maisha ya mtoaji huduma ni ya aina gani. Kunapotokea majanga kama vile mafuriko, mitetemeko ya ardhi au mikurupuko ya magonjwa watoa huduma za kibinadamu huonyesha ukakamavu mkubwa wanapoingia sehemu zilizoathirika na kuwahudumia wale walioathiriwa na majanga hayo. Mwandishi wetu wa Nairobi Jason Nyakundi ametuandalia makala kuhusu maisha na kujitolea kwa watoa huduma za kibinadamu kwenye kazi zao ngumu, Je kuna wakati wanahisi kuchoka na kukata tamaa? Ni changamoto zipi zinazowakabili?
amepata fursa ya kuzungumza na kanali mstaafu Nathan Kigotho kutoka kituo cha kitaifa cha kushughulikia majanga nchini Kenya yaani National Disaster Operations Center kutaka kuelewa zaidi kuhusu suala hili. Wasikilize.
MAHOJIANO NA KANALI KIGOTHO
Na sasa tunapata maoni kutoka kwa wanachi wa Tanzania , wanasemaje?
MAONI
Nao wananchi wa Burundi wana yapi ya kusema?
MAONI