Serikali ya Syria yatakiwa kusitisha ghasia mara moja
Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa na muungano wa nchi za kirabu nchini Syria Kofi Annan amesema kuwa serikali ya Syria ni lazima iwe ya kwanza kutangaza usitishaji wa ghasia na iondoe wanajeshi wake kutoka sehemu waliko raia.
Annan anasema kuwa anataraji nao upinzani kuchukua mkondo huu mara moja ikiwa ni moja ya yale yaliyopendekezwa na mjumbe huyo kwa lengo la kumaliza mzozo wa kisiasa ulio nchini Syria.
Annan amesema kuwa hata kama serikali ya Syria imeitikia mpango huo sasa ni lazima iutekeleze .
Hata hivyo ameongeza kuwa hakuna dalili za kuonyesha kuwa pande husika zina mipango ya kumaliza ghasia zilizo nchini humo. Ahmed Fawzi ni msemaji wa Annan.
(SAUTI YA AHMED FAWZI)