Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ban akaribisha kuanza upya kwa majadiliano baina ya Serbia na Kosovo juu ya mzozo wa mpaka

Ban akaribisha kuanza upya kwa majadiliano baina ya Serbia na Kosovo juu ya mzozo wa mpaka

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amekaribisha kuanza upya kwa majadiliano yanayoungwa mkono na Umoja wa Ulaya baina ya Serbia na Kosovo juu ya mzozo wao wa muda mrefu kuhusiana na mpaka. Pande hizo sasa zimekubaliana kutekeleza maazio yaliyoratibiwa na Umoja wa Ulaya maazio ambayo yanafungua njia juu ya kufikiwa kwa suluhu ya kudumu.

Akiweka zingatio lake, Ban amesema kuwa anaamini pande zote zitafikia makubaliano ambayo yataleta mwanga mpya. Mzozo wa mpaka kwa pande zote mbili umekuwa kitovu cha machafuko ya mara kwa mara na kusabisha baadhi ya watu kupoteza maisha.