Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Uhamiaji kutoka pembe ya Afrika kwenda nchini Yemen waandikisha rekodi mpya

Uhamiaji kutoka pembe ya Afrika kwenda nchini Yemen waandikisha rekodi mpya

Idadi ya wakimbizi na wahamiaji waliowasili nchini Yemen kwa njia ya bahari ilifikia watu 12,545 mwezi uliopita ikiwa ndiyo idadi kubwa zaidi kuandikishwa na shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR kwa mwezi tangu lianze kuchukua takwimu hizo mwaka 2006.

Idadi hiyo ilifikisha idadi watu wote waliowasili nchini Yemen kuwa watu 84,656 kati ya mwezi Januari na Novemba mwaka huu ikiwa ni ya juu kuliko iliyoandikishwa mwaka 2009 ya watu 77,000. Melisa Fleming ni msemaji wa UNHCR.

(SAUTI YA MELISA FLEMING)