Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR yachapisha maelekezo kukabili utovu wa ustahamilivu na ubaguzi wa wageni wahamiaji

UNHCR yachapisha maelekezo kukabili utovu wa ustahamilivu na ubaguzi wa wageni wahamiaji

Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) limechapisha, kutoka Geneva, leo hii maelekezo maalumu ya kutumiwa kukabili matatizo ya ubaguzi wa rangi na chuki, dhidi ya wageni, matatizo ambayo husababisha watu kuhama na kuhatarisha juhudi za UNHCR katika kuwapatia hifadhi watu waliokosa uraia, wahamiaji na wale wenye kuomba hifadhi za kisiasa.