Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Bagaragaza ahukumiwa kifungo cha miaka minane na ICTR kwa jinai ya halaiki Rwanda

Bagaragaza ahukumiwa kifungo cha miaka minane na ICTR kwa jinai ya halaiki Rwanda

Mahakama ya UM juu ya Rwanda (ICTR) imehukumu kifungo cha miaka minane kwa mtuhumiwa Michel Bagaragaza, aliyekuwa mfanya biashara mkuu katika Rwanda, kwa kushiriki kwenye mauaji ya halaiki yaliotukia nchini mwao katika 1994.