Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wahalifu wanane wa makosa ya vita Sierra Leone wahamishiwa kifungoni Rwanda

Wahalifu wanane wa makosa ya vita Sierra Leone wahamishiwa kifungoni Rwanda

Wahalifu wanane waliopatikana na hatia ya kushiriki kwenye jinai ya vita na makosa dhidi ya utu, na Mahakama Maalumu juu ya Makosa ya Vita katika Sierra Leone (SCSL), Ijumaa walisafirishwa kutoka vituo vya kufungia watu viliopo Freetown, Sierra Leone na kuhamishiwa kwenye Jela ya Mpanga, iliopo Kigali, Rwanda, kutumikia adhabu yao. Mahakama ya SCSL, inayoungwa mkono na UM, iliamua kuwapeleka wafungwa hawo wanane Rwanda kwa sababu magereza ya Sierra Leone hayatoshelezi viwango vya sheria ya kimataifa.