Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNICEF/WHO zimeanzsiha mradi wa kuzuia vifo vya watoto wachanga vinavyosababishwa na kuharisha

UNICEF/WHO zimeanzsiha mradi wa kuzuia vifo vya watoto wachanga vinavyosababishwa na kuharisha

Kadhalika, Shirika la UNICEF na Shirika la Afya Duniani (WHO) yameripotiwa kuanzisha mradi mpya wa pamoja, wenye makusudio ya kukinga na kuwatibu watoto na maradhi ya kuharisha - ikiwa ni ugonjwa wa pili wenye kusababisha vifo kwa wingi zaidi miongoni mwa watoto wachanga katika nchi zenye hali duni ya uchumi.