ICC imependekeza Bemba aachiwe kwa muda
Mahakama ya UM juu ya Makosa ya Jinai ya Halaiki (ICC) leo imetangaza kumwachia huru, kwa muda, aliyekuwa naibu-raisi wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Jean-Pierre Bemba Gombo mpaka wakati ambapo kesi yake itaanza kusikilizwa na mahakama.