Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Idadi ya wenye njaa kukiuka bilioni 1 duniani katika 2009, inasema FAO

Idadi ya wenye njaa kukiuka bilioni 1 duniani katika 2009, inasema FAO

Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) limetangaza jumla ya watu waliopo kwenye ukingo wa kubanwa na matatizo ya njaa ulimwenguni katika 2009, inakaribia watu bilioni 1.02 - sawa na sehemu moja ya sita ya idadi nzima ya watu duniani.