Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UM unaadhimisha Siku Kuu ya Watoto Duniani

UM unaadhimisha Siku Kuu ya Watoto Duniani

Tarehe 20 Novemba inaadhimishwa rasmi na UM kuwa ni Siku ya Watoto Duniani. Shirika la UM juu ya Mfuko wa Maendeleo kwa Watoto (UNICEF) limekaribisha, kwa nguvu kubwa, uamuzi wa baadhi ya vijana walioshiriki, katika siku za nyuma, kwenye mapigano wangali na umri mdogo, wa kuanzisha mtandao mpya utakaotumiwa kuamsha hisia za umma wa kimataifa juu ya shida wapatazo watoto kwenye maeneo ya migogoro na mapigano.