BU linasailia maendeleo Usomali
Baraza la Usalama, leo asubuhi, vile vile limezingatia ripoti ya KM juu ya hali katika Usomali. Miongoni mwa masuala yaliojadiliwa ni pamoja na hali ya usalama nchini, haki za binadamu na athari za kiutu kwa umma wa Usomali kutokana na kupwelewa kwa utekelezaji wa mapatano ya Djiboouti yaliofikiwa baina ya Serikali ya Mpito na Umoja wa Makundi ya Ukombozi wa Pili wa Usomali.