Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Siku ya Kimataifa Dhidi ya Kutumia Nguvu

Siku ya Kimataifa Dhidi ya Kutumia Nguvu

Alkhamisi, tarehe 02 Oktoba imeadhimishwa rasmi na UM kuwa ni Siku ya Kimataifa Dhidi ya Kutumia Nguvu, tarehe ambayo inalingana na sikukuu ya kuzaliwa kwa Mahatma Gandhi, kiongozi aliyegombania uhuru wa Bara Hindi kwa kufuata sera ya falsafa alioibuni, yenye kutilia mkazo mapambano ya kutotumia nguvu na wanaokandamiza.