D’Escoto apendekeza demokrasia irudishwe tena kwenye UM
Raisi wa kikao cha 63 cha Baraza Kuu la UM, Miguel D’Escoto kwenye mazungumzo na Redio ya UM pamoja na Kituo cha Habari cha UM alihimiza kwa kusema kwamba wakati umewadia kwa Mataifa Wanachama kuhakikisha demokrasia inarudishwa tena katika kuendeleza shughuli za UM.