Wapatanishi wa pande nne waisihi Israel na Wafalastina kujadiliana kiini cha mvutano wao
Kundi la kimataifa la wapatanishi wa pande nne wanaohusika na suluhu ya amani katika Mashariki ya Kati, ambao walikutana Makao Makuu ya UM Ijumaa, lilitoa mwito maalumu unaowataka WaFalastina kuahidi kukomesha vitendo vya kutumia mabavu na kuitambua Israel.