Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNEP imeshirikiana na Uchina kuandaa Olimpiki rafiki kwa mazingira

UNEP imeshirikiana na Uchina kuandaa Olimpiki rafiki kwa mazingira

Achim Steiner, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la UM juu ya Hifadhi ya Mazingira (UNEP) anatarajiwa kuhudhuria Sherehe za Ufunguzi wa Michezo ya Olimpiki mjini Beijing, Uchina mnamo tarehe 08 Agosti (08). Ziara hii ni kuthibitisha uungaji mkono wa UNEP zile juhudi za Uchina kuendesha mashindano ya olimpiki kwa kulingana na taratibu za kuimarisha hifadhi bora ya mazingira.