Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Sampuli za 'plutonium' kudhibitiwa baada ya kuvuja kwenye lebu ya IAEA

Sampuli za 'plutonium' kudhibitiwa baada ya kuvuja kwenye lebu ya IAEA

Shirika la UM juu ya Matumizi ya Amani ya Nishati ya Kinyukilia Kimataifa (IAEA) limeripoti Ijumapili kijichupa kidogo kilichofungwa kwenye maabara ya kuhifadhia sampuli za utafiti na ukaguzi, iliopo kwenye mji wa Seibersdorf, Austria kilifura shinikizo na kuvuja ile sumu kali ya maadini yanayojulikana kama plutonium, ambayo hutumiwa kutengenezea silaha za nyuklia.