Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Wataalamu wa mazao wakutana Vienna kutahminia taratibu mpya za kukithirisha mavuno

Wataalamu wa mazao wakutana Vienna kutahminia taratibu mpya za kukithirisha mavuno

Mashirika ya UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) na pia Matumizi ya Amani ya Nishati ya Nyuklia (IAEA) yametayarisha warsha maalumu mjini Vienna, Austria ambao unafanyika kuanzia tarehe 12 Agosti mpaka 15, kuzingatia taratibu mpya za kurekibisha uzalishaji wa mimea, mpango unaotarajiwa kukuza mavuno kwa wingi kusaidia nchi masikini. Kama inavyoeleweka katika miezi ya karibuni makumi milioni ya umma wa kimataifa wanakhofiwa huenda wakazama kwenye janga la njaa na ufukara kwa sababu ya mgogoro wa chakula na nishati ulimwenguni.