'Maamuzi ya G8 yanabashiria dalili njema, lakini kinachohitajika ni vitendo pia', asema Ban
Baada ya Mkutano Mkuu wa G8 kumalizika kwenye Kisiwa cha Hokkaido, Ujapani KM Ban Ki-moon alinakiliwa akisema kuwa anaunga mkono maamuzi ya viongozi wa G8 kuhusu ile mizozo mitatu iliofungamana kimataifa, na ambayo husumbua sana umma wa ulimwengu hivi sasa, yaani tatizo la athari za mabadiliko ya hali ya hewa, upungufu wa akiba ya chakula na mzoroto wa shughuli za maendeleo katika nchi maskini.