Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

FAO inasema mabadiliko ya hali ya hewa huathiri vibaya uvuvi

FAO inasema mabadiliko ya hali ya hewa huathiri vibaya uvuvi

Shirika la UM juu ya Chakula na Kilimo (FAO) limeonya wiki hii kwamba kuongezeka kwa hali ya joto, na mageuzi mengine kwenye mazingira yanayosababishwa na mabadiliko ya hali ya hewa, ni mambo yatakayoathiri, kwa uzito mkubwa zaidi, uvuvi pamoja na utamaduni wa shughuli za baharini. Kadhalika mabadiliko haya pia hunyima akiba ya chakula fungu maalumu la umma wa kimataifa unaotegemea mavuno ya uvuvi kuishi.