Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mahakama ya Makosa ya Vita Sierra Leone iwe funzo kwa kesi za viongozi wakosa

Mahakama ya Makosa ya Vita Sierra Leone iwe funzo kwa kesi za viongozi wakosa

Stephen Rapp, Mwendesha Mashitaka Mkuu wa Mahakama maalumu ya Jinai ya Vita katika Sierra Leone aliwaambia waandishi habari kwamba kesi ya kumhukumu aliyekuwa Raisi wa Liberia Charles Taylor inaendeshwa kwa utaratibu wa kufanyiwa mfano, ambao utawafalia wanasheria kuusoma ili kuona namna haki inavyotekelezwa katika sheria za kimataifa kwa viongozi waliokiuka mipaka wakati wakitawala. Alidai kwamba kesi ya mtuhumiwa aliyekuwa raisi wa Liberia, inaonyesha kwamba kesi kama hizo zinaweza kuendeshwa kwa uwazi, bila ya upendeleo, na hata kumpatia mtuhumiwa fursa halali ya kujitetea. ~~