Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR imepungukiwa fedha za kuhudumia wahamiaji wa Sudan Kusini

UNHCR imepungukiwa fedha za kuhudumia wahamiaji wa Sudan Kusini

Jennifer Pagonis, Msemaji wa Geneva wa Shirika la UM juu ya Huduma za Wahamiaji (UNHCR) ameripoti kwa waandishi habari kuwa taasisi yao inakabiliwa na upungufu wa dola, karibu milioni 12, zinazotakiwa kushughulikia operesheni za kuwasaidia kihali wahamiaji wa Sudan Kusini waliodhamiria kurudi mwakao katika nusu ya pili ya mwaka. Huduma hizi zikikamilishwa zitawapatia wahamiaji hawo uwezo wa kuanzisha maisha mapya.

Sikiliza taarifa kamili kwenye idhaa ya mtandao.