Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Radovan Karadzic awekwa rumande Hague kwenye kituo cha UM

Radovan Karadzic awekwa rumande Hague kwenye kituo cha UM

Radovan Karadzic Ijumatano asubuhi alihamishwa kutoka Serbia, eneo aliokamatwa mnamo tarehe 21 Julai 2008, na amepelekwa kizuizini mjini Hague, Uholanzi penye Kituo cha Kufungia Watu cha UM. Nerma Jelacic, Msemaji wa Mwendesha Mashitaka wa Mahakama ya UM juu ya Yugoslavia ya Zamani (ICTY) alithibitisha taarifa hiyo kwenye mazungumzo na Redio ya UM.~