Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

OHRC inaitaka Misri isitishe kufukuza nchi WaEritrea

OHRC inaitaka Misri isitishe kufukuza nchi WaEritrea

Louise Arbour, Kamishna Mkuu wa Ofisi ya UM juu ya Haki za Binadamu (OHRC), ameripoti "kushtushwa sana" na taarifa zinazothibitisha ya kuwa katika siku za karibuni taifa la Misri limefukuza na kuondosha nchini wahamiaji 700 wa kutoka Eritrea, walikuweko nchini humo wakisubiri jawabu ya maombi yao ya kupatiwa hifadhi ya kisiasa.