Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

BU kulaumu mashambulio ya JEM dhidi ya Serikali Sudan

BU kulaumu mashambulio ya JEM dhidi ya Serikali Sudan

Ijumanne Raisi wa Baraza la Usalama kwa mwezi Mei, Balozi John Sawers wa Uingereza aliwaarifu waandishi habari kwamba wajumbe wa Baraza wamekubaliana kushtumu vikali, kwa kauli moja mashambulio ya silaha dhidi ya Serikali yalioendelezwa na wafuasi wa kundi la waasi wa Darfur la JEM katika tarehe 10 Mei kwenye eneo la Omdurman, kitongoji kilichopo nje ya mji mkuu wa Khartoum, Sudan.