WHO inawakumbuka waliofariki maafa maumbile Myanmar/Uchina
Kwenye ufunguzi wa kikao cha mwaka cha Baraza Kuu la Shirika la Afya Duniani (WHO) mjini Geneva leo Ijumatatu wajumbe wa kimataifa kutoka nchi 193 walijumuika kuwakumbuka watu waliofariki kwenye Kimbunga Nargis nchini Myanmar, na vile vile wale watu walioangamizwa na zilzala iliopiga Uchina majuzi. Wajumbe wa WHO walikaa kimya kwa dakika kuwakumbuka waliokufa.~~