Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Naibu Kamishna Mkuu juu ya Haki za Binadamu azuru Cote d'Ivoire na Liberia

Naibu Kamishna Mkuu juu ya Haki za Binadamu azuru Cote d'Ivoire na Liberia

Naibu Kamishna Mkuu wa UM juu ya Haki za Binadamu, Kyung-wha Kang wiki hii ameanza ziara maalumu, ya pili, katika mataifa ya Cote d\'Ivoire na Liberia ambapo atafanya mazungumzo na viongozi wenye mamlaka, makundi yanayowakilisha jumuiya za kiraia, pamoja na wanadiplomasiya, na vile vile watumishi wa vyeo vya juu wa UM na kushauriana nao kuhusu hatua za kuchukuliwa kipamoja, zitakazohakikisha kadhia ya kuhifadhi haki za raia itatumiwa kuwa ni kipengele muhimu cha upatanishi miongoni mwa makundi yanayohasimiana, na pia katika kufufua kadhia za kiuchumi na jamii kwenye mataifa husika.