Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mkutano wa Durban unazingatia hifadhi bora dhidi ya utumwa mamboleo

Mkutano wa Durban unazingatia hifadhi bora dhidi ya utumwa mamboleo

Shirika la Kimataifa juu ya Uhamaji (IOM) limeripoti kukutana katika mji wa Durban, Afrika Kusini waundaji sera kadha wa kadha pamoja na viongozi wa serikali kutoka mataifa ya kusini mwa Afrika, kwa madhumuni ya kuzingatia namna ya kuandaa taratibu za kuwakinga raia wanaotoroshwa na kupelekwa mbali na makwao kuhudumia vibarua haramu, mathalan, umalaya au ajira isio ya kulazimishwa isiokuwa na malipo. Mkutano unatarajiwa kuendelea kwa siku tatu.