Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Ukosefu wa nishati wailazimisha UNRWA kusitisha misaada Ghaza

Ukosefu wa nishati wailazimisha UNRWA kusitisha misaada Ghaza

Shirika la UM linalosimamia Huduma za Kiutu katika Maeneo ya Wahamiaji wa Kifalastina Mashariki ya Kati, UNRWA, limeripoti na kuthibitisha kwamba limesitisha kupeleka chakula kwa umma muhitaji waliopo kwenye Tarafa ya Ghaza, kwa sababu ya ukosefu wa petroli inayohitajika kutumiwa kwenye malori yanayotumiwa kugawa misaada hiyo.