Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

UNHCR imesitisha misaada katika JKK baada mapigano kufumka

UNHCR imesitisha misaada katika JKK baada mapigano kufumka

Ron Redmond, Msemaji wa Shirika la UNHCR aliwaambia waandishi habari Ijumaa mjini Geneva kwamba shirika lao limelazimika kusitisha ugawaji wa misaada ya kihali kwa wahamaji wa ndani ya nchi waliopo Jimbo la Kivu Kaskazini, katika JKK, baada ya kuzuka tena mapigano mapya katika eneo hilo. Hata hivyo, UNHCR bado inaendelea kuisaidia Serikali ya JKK kusajili wahamaji wanaomiminikia katika eneo la Rutshuru liliopo kilomita 70 kaskazini ya mji wa Goma. Idadi ya wahamaji wa ndani ya nchi waliopo Kivu Kaskazini kwa hivi sasa inakadiriwa 860,000.