Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Siku ya Malaria Duniani

Siku ya Malaria Duniani

Kwa mara ya kwanza katika historia jamii ya kimataifa imeamua kuiheshimu tarehe 25 Aprili kila mwaka kuwa ni Siku ya Malaria Duniani. UM na mashirika yake kadha wa kadha yameandaa tafrija na hafla aina kwa aina ili kukumbushana juhudi zinazotakikana kutekelezwa kwa ushirika miongoni mwa Mataifa Wanachama, ili kufanikiwa kudhibiti bora maradhi ya malaria kote duniani.