Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

BK linajadilia taratibu za kupunguza ajali za barabarani duniani

BK linajadilia taratibu za kupunguza ajali za barabarani duniani

Ijumatatu Baraza Kuu la UM limeitisha kikao maalumu, cha wawakilishi wote, katika Makao Makuu ili kuzingatia usalama barabarani baada ya ripoti ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kuonya ya kuwa athari zinazotokana na ajali za barabarani zimeanzisha “mgogoro mpya wa hatari, kwa afya ya jamii” takriban kote duniani. Kwa mujibu wa ripoti ya WHO athariza za ajali za barabarani zinalingana na madhara yanayotokana na maradhi ya kifua kikuu, malaria na UKIMWI dhidi ya umma wa kimataifa.