Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Madereva wa huduma za maji Darfur waachiwa huru na majambazi

Madereva wa huduma za maji Darfur waachiwa huru na majambazi

Shirika la UNICEF limeripoti faraja mwisho wa wiki iliopita baada ya kupokea taarifa kuhusu kuachiwa huru wale madereva wanne, watumishi wa Shirika la Maji la Sudan waliotekwa nyara wiki mbili nyuma katika jimbo la vurugu la Darfur Kaskazini. Madereva wanne hawa hivi sasa wamesharejeshwa kuungana na aila zao. Lakini vile vifaa vya thamani vilivyobebwa kwenye magari ya madereva wa Shirika la Maji la Sudan havijapatikana tena na vimepokonywa na maharamia. Huduma shirika za za maji zinazotekelezwa na Shirika la Maji la Sudan pamoja na UNICEF katika Darfur Kaskazini huwasaidia makumi elfu ya raia wa eneo hilo kupata maji safi ya kunywa na matumizi ya nyumba.