Mjumbe wa KM ahimiza majadiliano kuharakisha amani Darfur
Mkutano wa kuleta amani kwenye eneo la vurugu la Darfur, Sudan ulifunguliwa rasmi Ijumamosi kwenye mji wa Sirte, Libya. Katika mahojiano na waandishi habari kwenye ukumbi wa mkutano Mjumbe Maalumu wa KM kwa Darfur, Jan Eliasson alisema ya kuwa, kwa makadirio yake yeye binafsi, anaamini asilimia kubwa ya makundi husika na mgogoro wa Darfur yaliwakilishwa vizuri mkutanoni na ana matumaini mema juu ya kikao cha Sirte:~~