Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

MONUC inasema "vikosi vya Serekali DRC vinakiuka haki za binadamu"

MONUC inasema "vikosi vya Serekali DRC vinakiuka haki za binadamu"

Ripoti ya Shirika la UM la Ulinzi wa Amani katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (MONUC) juu ya utekelezaji wa haki za binadamu katika Kongo-DRC kwa Julai imeshtumu vikali vitendo vya wanajeshi wa Serekali, baada ya kuthibitisha kwenye uchunguzi wao kwamba vikosi hivyo vimegunduliwa vikiharamisha haki za binadamu nchini kwa mapana na marefu, ambapo wanajeshi wamekutikana wakiua raia kihorera, wakinajisi wanawake kimabavu, na kuendeleza wizi na dhulma, na kunyanganya raia mali zao.