Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Mataifa Wanachama yakutana mjini Paris kuzingatia ukomeshaji wa matumizi ya watoto katika mikwaruzano ya vita

Mataifa Wanachama yakutana mjini Paris kuzingatia ukomeshaji wa matumizi ya watoto katika mikwaruzano ya vita

Mnamo mwanzo wa wiki wawakilishi kutoka mataifa wanachama 58 walikutana kwa siki mbili katika mji wa Paris, Ufaransa kwenye mkutano uliopitisha itifaki ya kukomesha, kote ulimwenguni, tabia karaha na vitimbi haramu vya kuajiri kwa nguvu watoto wanaolazimishwa kushiriki katika vita na mapigano.