Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Naibu KM mpya aahidi usimamizi wa kazi za UM kwa nidhamu za fungamano

Naibu KM mpya aahidi usimamizi wa kazi za UM kwa nidhamu za fungamano

Ijumatatu, Februari 05 (2007) Asha-Rose Migiro, aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Nje na Maendeleo wa Tanzania aliapishwa rasmi kuwa Naibu KM mpya wa UM. Baada ya Bi Migiro kuapishwa na kutia sahihi waraka za UM alijulishwa na KM Ban Ki-moon na waandishi habari wa kimataifa waliopo Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa. Naibu KM Migiro aliwaambia wanahabari hawo kwamba atajitahidi kama awezavyo kuziongoza kazi za UM kwa nidhamu iliyoungana, na kwa taratibu zinazoeleweka kwa masilahi na natija za taasisi hii pekee ya kimataifa.