Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Hali katika Iraq yatia wasiwasi

Hali katika Iraq yatia wasiwasi

KM ameonya kwamba hali ya usalama, kwaujumla, katika Iraq imefikia ‘kikomo cha hatari’ na inabashiria kuzusha mapigano ya wenyewe kwa wenyewe miongoni ya makundi yenye uhasama wa kimadhehebu nchini humo. Kwa mujibu wa takwimu za Serekali imethibitika kwamba kila siku watu 100 huuawa nchini Iraq na, kwa wastani, 14,000 wengineo hujeruhiwa kila mwezi.